TESTIMONIES

                 
       
Naitwa ABRAHAM ALFRED ni Mkazi wa mfulu Morogoro nina umri wa miaka 56 na kikabila mimi ni Mnyamwezi, Matatizo yangu yalianza muda kidogo siku moja  nilivyoamka asubuhi nilihisi ganzi katika miguu yangu baada ya siku kadhaa ganzi hiyo iliendelea hadi kufika Kiunoni hapo ndipo hali yangu ilikuwa mbaya sana sikuweza kutembea peke yangu vizuri kama zamani, pia hata nilibidi nisimame kufanya kazi kutokana na matatizo yaliyo nitokea hali ilizidi kuwa mbaya ndipo nilipo amua kwenda Hospitali ya mkoa Morogoro ili kuchukua vipimo , Nilipofika nilipima vipimo vya PRESHA, HIV na XRAY na baada ya vipimo niligundulika na magonjwa ya SUKARI , PRESHA, FIGO YA KULIA ILIKUWA IMEKUFA, INI HALIFANYI KAZI, Na madaktari waliniambia hata ganzi niliyokuwa nayo ilisababishwa na hayo magonjwa kwahiyo nilipewa dawa za kutumia lakini hazikufanya kazi na hali ilizidi kuwa mbaya zaidi , Ndugu zangu wa kristo hapo ndipo niliamua kwenda kwa waganga wa kienyeji. Nilipita kwa waganga takribani 18 wa hapa Morogoro kujaribu kutafuta msaada wa hali ya afya yangu lakini nilipoteza Pesa nyingi na sikuona unafuu wowote bali nilizidi kupata shida.

Ndipo siku moja Kuna jirani yangu mmoja alikuja kunihubiria habari za yesu na kunishauri niende naye katika ibada siku ya ijumaa tarehe 19/02/2016 Nilikubaliana naye na siku hiyo nilikwenda kanisani(EFATHA MINISTRY MOROGORO) Wakati wa maombezi ulipofika nivyoombewa nilianguka baada ya hapo nilianza kuhisi ile ganzi miguuni ikianza kuondoka katika miguu yangu. Na ndipo mchungaji (GLADNESS TUPA) Akaniamuru “NITEMBEE” Niliamka kwa Imani na kuanza kutembea na kukimbia na kucheza nyimbo za dini zilizokuwa zikipigwa wakati ule, Nilifurahi sana na kumshukuru MUNGU kwa aliyonitendea “KWAKWELI SITA MUACHA HUYU YESU.



NAITWA UPENDO MWAKYUSA: 
Namshukuru MUNGU kwa matendo makuu aliyonitendea kwa habari ya maisha yangu, toka nilipozaliwa sikumfahamu mama yangu, na baba yangu kwani walifariki nikiwa mdogo sana. Napenda kumshukuru Mungu Aliye Baba wa yatima, amenipa wazazi wazuri Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira na Mama Eliakunda, wamenilea mpaka sasa niko hapa ni wao wamenilea. Na kwa habari ya elimu yangu Mwaka 2012 nilipata neema ya kusoma Muhimbili na NENO la Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii aliniambia nitatoboza na sasa nimemaliza masomo yangu vizuri namshukuru Mungu. Kwa habari ya afya yangu tangu nilipokuwa mdogo nilikuwa ninaumwa kichwa na kifua, na niliambiwa katika ukoo wetu ni kawaida kuumwa hivyo, na nilikuwa ninatumia dawa nikadhani kuwa maisha yangu yote ndiyo nitakuwa natumiadawa kila siku. Toka mwaka 2012 nilisikia mama moja anatoa ushuuda hapa Efatha ameponywa kichwa na kifua, nikamwambia MUNGU na mimi napokea, toka siku hiyo mpaka leo sijawahi kuumwa tena wala kutumia dawa tena. Namrudishia sifa na utukufu MUNGU wa Efatha.