MCH. RICKY MONGI
Mwaka wa mtembeo wa mng`ao ni mwaka wa kutembea na
kuwa na majukumu maana mng`ao ni majukumu hivyo mtu mvivu mzembe asiye na chakufanya hawezi kung`aa maana penye mng`ao
pana majukumu maana kuwa na Mungu nikuwa na majukumu.
Huu sio wakati wa kupoteza muda maana penye nuru
pana majukumu , Na kazi ya nuru ni
Kuongeza, kustawisha, kuchanusha.
Mtu wa Mungu ni mtu wa majukumu na nuru ni majukumu
na kukubali kutembea na mng`ao ni majukumu
Luka 8:16
Jukumu la nuru ni kuwaonyesha na kuwaangazia
wanaoingia wajue cha kufanya
Jukumu ya nuru ni kuwapa ulinzi waingiao hivyo nuru
ina majukumu na wewe pia unapaswa kuwa na majukumu
Taa siku zote inawekwa juu kwa sababu ina jukumu la
kuangaza na taa isiyoangaza siku zote
inashushwa jiulize wewe una
jukumu gani litakalokufanya uinuliwe juu usishushwe tena?
Mathayo 5:14-16
Maana Mungu wako atatukuzwa kwa jukumu unalolifanya
na siku zote hutahitaji kushuhudia maana jukumu lenyewe linamuuza Yesu
Kwasababu wewe ni nuru tena unaangaza kuna vitu
utafanya vitakua sababisha wengine kuiga kutoka kwako maana nuru yako
inatakiwa kuangaza mbele za watu
Kazi unayoifanya, biashara unayoifanya shuhuli
yoyote unayoifnya unapaswa uwe zaidi ya wengine kwasababu wewe ni nuru
Mtu wa nuru
ni kiongozi kwa wengine maana nuru huwa inatuongoza
Mtu wa nuru ni mtu wa kuonyesha njia maana nuru
inatuangazia
Mtu wa nuru anapaswa kuigwa na wengine
Mtu wa nuru anafanya kitu cha tofauti na wengine
Mtu wa nuru hapaswi kujidharau, kukiri udhaifu
na kushindwa
Isaya 42:6-7
Kuwafungua macho vipofu yaani kufanya mambo ambayo
wengine walikuwa hawayaoni bali sasa wanaona kupitia wewe
YOHANA 11:9-17
Haiwezekani ukafungua biashara au kufanya kitu
chochote katika mwaka huu wa mng`ao halafu kikakwama
Leo jiulize lazaro ni kipi katika maisha yako? kipi
kimekufa Katika maisha yako? lakini kwa haijalishi chochote ulichonacho
kimekufa siku ngapi kwa mamlaka ya jina la Yesu chochote kilichokufa kama
lazaro lazima anaenda kufufuka