IBADA YA SEMINA  Trh 19/02 /2015 - 23/02 /2015

SIKU YA KWANZA


Somo: FAMILIA KAMA LANGO
Maana ya lango
Yohana 10:9
Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Katika Yohana 10:7 Bibia inasema;“Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.”

Kuna mlango ukiingia sahau wokovu na Kuna mlango ukiingia kuna utele, utele wa Maisha, Baraka, Amani, uzima n.k. Huu ndiyo mlango wa Yesu Kristo.

Tunaweza kuona katika Yohana 10:10;Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Mtu alivyo nia sawasawa na mlango alikotokea.
Tuangalie sasa lango katika kiwango cha familia
Mwanzo 49:1-
1.      Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho.
2.      Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu.
3.       Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu.
4.      Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, Kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako, Ukakitia unajisi; alikipandia kitanda changu.
Kuna mambo hayatafutwi chuoni au kwa kuwa na elimu, bali mtu huyapata katika familia aliyozaliwa, mfano UKUU na NGUVU.
Mwanzo 47:7
Yusufu akamleta Yakobo babaye ndani akamweka mbele ya Farao Yakobo akambariki Farao.
(Ndivyo ilivyo katika familia zingine, watu wakuja hubarikiwa na kuacha wa ndani bila mibaraka).
Mwanzo 29:20-25
20.  Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa vile alivyompenda.
21.  Yakobo akamwambia Labani, Nipe mke wangu, maana siku zangu zimetimia; niingie kwake.
22.  Labani akakusanya watu wote wa mahali pale, akafanya karamu.
23.  Ikawa wakati wa jioni akamtwaa Lea, binti yake, akamletea Yakobo, naye akaingia kwake.
24.  Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake.
25.  Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda?
Hapa tunaweza kuona kuwa katika familia nyingi ni wengi wameoa akina lea badala ya Raheli, Kutokana na changamoto za mazingira, masomo, utajiri n.k. watu wamebadili mitazamo yao na kuoa wanawake wasio wa kwao!!
Angalia familia ya yakobo ilivyoishi
Mwanzo 30:14-15
14.  Reubeni akaenda siku za mavuno ya ngano akaona tunguja kondeni, akazileta kwa Lea mamaye. Ndipo Raheli akamwambia Lea, Nipe mimi baadhi ya tunguja za mwanao.
15.  Naye akamwambia, Je! Ni jambo dogo kuninyang'anya mume wangu; hata wataka kuzitwaa tunguja za mwanangu pia? Raheli akamwambia, Kwa hiyo atalala kwako usiku huu kwa tunguja za mwanao.
Hapa utaona kuwa familia haikuwa na Amani kutokana na Yakobo kumwoa Lea kwanza badala mke wa agano lake Raheli.
Siyo sawa kuwalaumu wazazi maana hujui yale waliyoyapitia mpaka kufikia hapo walipo, maana mtu huweza kupitia mambo yakambadilisha na kuyafanya yaliyo kinyume na kusudi la kuumbwa kwake. Tunaona katika mwanzo 30:1-13, ambapo Yakobo alijikuta anakuwa na wanawake wane badala ya mmoja Raheli aliyekuwa wa agano naye. Maamuzi haya yalitokana na Yakobo kukosa UTHABITI katika MAISHA baada ya kutendwa. Ndipo utendaji wake, mawazo yake, maamuzi yake na mfumo wake mzima wa maisha ulipobadilika hata kufikia kutoa laana kwa mwanae Reubeni.

Share this